Ndanda

Kitengo cha Endoscopy

Kitengo chetu cha endoscopy kina mashine za kisasa ambazo hutumia camera inayowezesha kuingia katika tumbo, utumbo mdogo na utumbo mkubwa, pia inatuwezesha kuingina ndani ya mapafu. Tunatumia minara miwili ya endoscopy yenye gastroscopes tano,colonoscopes mbili na bronchoscope moja. Huduma hizo hutolewa katika vyumba vipya vilivyofanyiwa ukarabati na mazingira mazuri kwa wagonjwa wetu na wafanyakazi wetu. Endoscopies hufanywa na mtaalam mmoja na timu yake,inayojumuisha madaktari wawili wa matibabu (MD) na wauguzi 6 wa endoscopy. Timu hiyo ilipata mafunzo na wataalam wakuu kutoka Ujerumani. Wengine wamepata mafunzo Idara ya Endoscopy ya Hospitali ya Taifa Muhimbili Dar Es salaam. 

Tunatumia endoscopy ya kisasa ya video ambayo ina uwezo wa kufanya uchunguzi na taratibu mbalimbali wakati wa huduma. Baadhi ya magonjwa tunayoyagundua  ni pamoja na ugonjwa wamaambukizi ya tumbo, vidonda vya tumbo, mishipa ya koo au tumbo, Kansa ya koo, tumbo na utumbo mkubwa.   Wagonjwa wengine wanagunduliwa kuwa na uvimbe wa utumbo. Zifuatazo ni huduma zitolewazo baada ya kugunduliwa,kuondoa kitu kisicho hitajika mwilini,kuunganishwa kwa mishipa ya damu,kuchomwa sindano ya adrenalini kwenye mishipa ya damu, kutoa uvimbe usiohitajika,utanuzi wa ndani ya mfumo wa chakula, ERCP inafanywa na wataalam wakuu wakati wa kambi za endoscopy. Sampuli hutolewa kama inahitajika na majibu hupatikana ndani ya wiki mbili. Idadi ya endoskopies zilizofanywa katika hospitali yetu imeongezeka kutoka 187 mwaka 2018 hadi 1043 mwaka 2021 na inaendelea kuongezeka.Mahitaji ya uchunguzi huu ni mkubwa kwasababu kuna maambukizi makubwa ya magonjwa bila kugunduliwa ya njia ya utumbo katika mikoa inayotuzunguka Ndanda na katika ukanda wa kusini mwa Tanzania. Ndanda ndiyo Hospitali pekee itoayo huduma hizi maalum.