Kuanzia tarehe 20.2.2022 hadi tarehe 8.4.2022 Dr. Fritjof Schmidt-Hoensdorf na timu yake wametutembelea Ndanda. Wao ni wataalamu maalum wa upasuaji wa mguu kifundo uliodharauliwa. Watoto walio na mguu kifundo wanaweza kutibiwa kwa kufunga kopa kama matibabu yataanza mapema katika siku za kwanza au wiki baada ya kuzaliwa. Kwa wanaokuja wamechelewa sana kwa njia hii ya kufunga kopa wanapaswa kutibiwa kwa upasuaji maalumu. Matangazo kuhusu kambi hii yamefanywa kupitia mabango,vipeperushi na redio.Zaidi ya Wagonjwa 70 wamefika na wamechunguzwa na wataalamu.
Madaktari 5 wa upasuaji wa mifupa,watoa dawa ya usingizi 2, na wauguzi wa chumba cha upasuaji kutoka Ujerumani wakishirikiana na wafanyakazi wetu. Wamefanikiwa kufanya upasuaji wa wagonjwa 43 na baadhi yao wamepata upasuaji zaidi ya mmoja. Upasuaji kwa wagonjwa wote ulifanikiwa na baada ya muda wa kufanyiwa mazoezi watatembea kama kawaida. Mradi huu umeafadhiliwa na Interplast na shughuli zote zimefanywa bila malipo. Sambamba na timu ya mguu kifundo, Sambamba na timu ya mguu kifundo , Dr Sevior,daktari wa ngozi kutoka Afrika ya kusini alifika kwa muda wa wiki moja. Wagonjwa wenye shida ya ngozi,wameshauriwa na kutibiwa kwa mafanikio.