Hospitali ya rufaa ya Mtakatifu Benedicto Ndanda inajulikana sana katika eneo lote la kusini mwa Tanzania. Ni hospitali ya binafsi ya kidini na sehemu ya shughuli za kitume za Abasia ya Ndanda. Lengo letu ni kutoa huduma bora za afya kwa wagonjwa wote,bila kujali imani ya mtu, hali ya kijamii na kiuchumi. Timu yetu ina wafanyakazi 338, ikijumuisha wataalam 6, Madaktari 10 (MD),Madaktari wasaidizi 3 (AMO), Madaktari 8 wa ndani na wauguzi 102,Wagonjwa wanatoka mikoa ya mbali ikiwemo Dar es Salaam, ya Zanzibar na Msumbiji. Kwa wagonjwa wa kulazwa tuna vitanda rasmi 300 ndani ya wodi 12 tulizonazo. Kwa mwaka tunawahudumia wagonjwa wa nje zaidi ya 80.000 wakiwemo wagonjwa wa ndani zaidi ya 7.000.
Tunatoa huduma za kimsingi na maalum kwa kutumia vifaa vya kisasa. Maabara yetu ina vifaa vya kutosha na imepata nyota 5. Tuna kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU),NICU na uchujaji damu (dialysis) yenye mashine 10 za uchujaji damu. CT Scan, Mashine ya X-ray ya kidijitali,Mashine za upigaji picha za hali ya juu (U/S) na endoscopy ya video zinatumika. Wafanyakazi wetu wamefundishwa vyema na kuhamasishwa sana kutoa huduma bora zaidi.
Kuanzia tarehe 21/4/2022 hadi tarehe 23/4/2022, Dk. Winfried Grasbon, daktari bingwa wa macho kutoka Ujerumani ametutembelea tena Ndanda.
Tarehe 26.2.2022 mtambo wa kujaza oksigeni uliwasili Ndanda Hospitali. Ufungaji ulianza mara moja na makabidhiano yalifanyika tarehe 4.3.2022.
Ukarabati
Wodi zetu zilijengwa kati ya mwaka 1965 na 1970, kwa sasa hazikidhi mahitaji na viwango. Mwezi wa tisa mwaka 2021, tulifanikiwa kuanza ukarabati wa wodi ya upasuaji ya wanaume,choo kimoja na korido.