Ndanda

Idara ya magonjwa ya kinamama.

Kitengo cha magonjwa ya wanawake ni moja ya kitengo kikubwa hapa hospitalini kwetu.Ni kitengo muhimu katika kushughulikia Afya ya Uzazi wa akina Mama  na baadhi ya Wanaume wenye tatizo la uzazi.

Hivi sasa kitengo hiki kinawatumishi 39 ambao wenye mori wa kufanya kazi kwa bidii kutoka kada mbalimbali nazo ni:

  • 1 Dkt Bingwa wa magonjwa ya wanawake
  • 1 Dkt Msajiliwa (MD)
  • 3 Madaktari wanafunzi (MD) Intern doctors
  • 17 Manesi Wasajiliwa
  • 13 Wauguzi
  • 4 Wauguzi wasaidizi

Kitengo kinatoa huduma kwa wagonjwa wa nje (OPD) wa Ndani (IPD) pamoja na Upasuaji.

WAGONJWA WA NJE[ OPD]

Kitengo hiki kinafanyakazi siku 5 kwa wiki,huduma zitolewazo ni pamoja na Afya ya Uzazi,huduma ya Mama na Mtoto RCH,uchunguzi wa saratani ya shingo ya kizazi pamoja na magonjwa yote ya Wanawake yahusuyo Uzazi.

HUDUMA ZA WAGONJWA WA NDANI[ IPD]

Huu ni mjumuhisho wa huduma za kujifungulia watoto, pia matunzo maalum hutolewa hasa kwa watoto wachanga wenye matatizo ya kiafya baada ya kuzaliwa.

Wamama wote walio jifungua watoto huwekwa wodini kwa masaa 24 kwa ajili ya uangalizi na uchunguzwaji wa karibu.

HUDUMA YA UPASUAJI

Huduma hii ya uzazi kwa njia ya upasuaji hutolewa kila siku na mda wowote inapotokea dharula ,lakini kwa kesi ambazo si za dharula hufanywa siku 4 katika wiki.