Ndanda

CT Scan

Makabidhiano ya Wodi ya Matibabu ya wanawake

Mnamo  tarehe  27/1/2023, Makabidhiano ya ukarabati wa Wodi ya matibabu ya kike (wodi tatu) pamoja na choo  yalifanyika. Malengo ya ukarabati huu ni kuwa na faragha zaidi kwa wagonjwa wetu,  kuwawezesha wauguzi kufanya ufuatiliaji wa karibu kwa wagonjwa wetu,  kuleta oksijeni na kuboresha usafi kwa wagonjwa wetu. Mbunifu wetu ameandaa ramani iliyofanana na wodi namba nne ambayo imekarabatiwa karibuni. Shukrani kwa michango ya wafadhili wetu, tumeweza kuanza ujenzi mwezi wa kumi 2022.

Faragha kwa wagonjwa wetu imepatikana kutokana na kujenga ukuta na kufunga mapanzia. Ufuatiliaji wa karibu wa wagonjwa unapatikana kupitia mfumo wa mawasiliano na sehemu maalumu ya muuguzi katika chumba, kuna vitanda viwili karibu na kituo cha wauguzi kwa ajili ya wagonjwa wanaohitaji uangalizi wa karibu zaidi. Kila kitanda kina vifaa vya kupata oksijeni, madirisha mapya yamewekwa  na taa za kisasa  za LED hutoa mwanga wa kutosha, chumba kimoja kimeandaliwa kwa ajili ya wagonjwa wenye maambukizo, chumba cha chai kwa waugzuzi, chumba cha daktari, ofisi ya muuguzi kiongozi, chumba cha kusafisha vifaa na stoo. Usafi umeimarishwa kwa  ukarabati wa choo pia kwa matumizi ya walemavu. Ukarabati wa wodi zilizokarabatiwa unathamaniwa sana na wagonjwa pamoja na wafanyakazi wetu. Tunawashukuru sana wafadhili wetu ambao wametuwezesha kufanikisha mradi huu.