Ndanda

Kambi za magonjwa ya mfumo wa chakula.

 Mnamo mwezi Septemba na Novemba mwaka 2021,kambi mbili za magonjwa ya mfumo wa chakula zinafanyika katika hospitali yetu.  Kuanzia tarehe 15 Septemba hadi tarehe 8 Octoba,Madaktari bingwa wa mfumo wa chakula kutoka Munich wametutembelea. Wameanzisha ERCP kwenye kituo chetu na huduma tatu zimefanyika kwa mafanikio. Pia wamefanya uchunguzi wa magonjwa ya tumbo na utumbo mkubwa kwa uingiliaji kati kama sindano ya adrenalini,kukatwa na kufunga. Mafunzo ya kina yametolewa kwa madaktari na wauguzi wetu.

 

    Kambi ya pili imefanyika kuanzia tarehe 1 hadi 28 Novemba 2021. Mtalamu wa magonjwa ya mfumo wa chakula Dr. Gatz na muuguzi wa uchunguzi wa mfumo wa chakula Bi. Ecke wametutembelea kwa mara ya tano. Matangazo yalifanyika kwa wagonjwa wa homa ya manjano, kutapika damu, kumeza, maumivu ya tumbo, damu kwenye kinyesi na magonjwa mengine walialikwa hospitalini kwetu. Wakati wa kambi, ERCP`s 13 zimefanywa kwa mafanikio pamoja na uchunguzi wa magonjwa ya njia ya chakula zaidi ya 130 pamoja na tumbo na hewa. Mafunzo ya kina kwa wafanyakazi wetu wa idara ya endoscopy yamefanywa, kwa hiyo ERCP imeimarika vizuri katika hospitali yetu madaktari na wauguzi wetu wa ndani wana uwezo mkubwa sana katika uchunguzi wa endoscopy.