Ndanda

Chanjo ya Korona

Tangu  tarehe 4/8/2021, chanjo dhidi ya UVIKO- 19 inapatikana katika Hospitali yetu ya Ndanda, haswa Chanjo ya JANSSEN-Covid 19 (Johnsen & Johnsen). Mahitaji ya chanjo ni makubwa, kwani nchi bado inakabiliwa na wimbi la tatu ugonjwa huu.
Vikundi vilivyopewa kipaumbele kwanza kupata chanjo ni wafanyakazi sekta ya afya, wagonjwa walio na magonjwa sugu na watu wenye umri kuanza miaka 50. Wakati huo huo, wateja wote zaidi ya umri wa miaka 18 wanaweza kupewa chanjo.

Chanjo ya JANSSEN-Covid 19 inahitaji sindano ya dozi moja tu.
Ulinzi wa kutosha dhidi ya ugonjwa hupatikana siku 14 baada ya sindano.
wafanyikazi wetu wengi tayari wamepokea chanjo hii na tunaendelea kutangaza huduma hii kwa wagonjwa wetu, ndugu na jamii.
Chanjo inatolewa bure.