Ndanda

CT Scan

Makabidhiano ya Wodi namba Nne

Wodi zetu zilijengwa kati ya mwaka 1965 na 1970. Tangu muda mrefu wodi zetu hazikuwa na viwango vya kisasa, hivyo ukarabati unahitajika kwa haraka. Asante kwa mchango wa ukarimu kutoka kwa Bi.Kleiner,Mindelheim wa Ujerumani, katika ukumbusho wa marehemu mume wake Bw. Ludwig Kleiner,tumefanikiwa kufanya ukarabati wa kina wa wodi namba nne ambayo ni ya kiume magonjwa ya kawaida. Lengo ni kuwapa usiri zaidi wagonjwa wetu, kuweza kufuatilia kwa ukaribu zaidi huduma tuzitoazo kwa wagonjwa wetu, kuweka vifaa vya oksijeni kwa kila kitanda, pia kuweka mwanga wa kutosha na kuboresha usafi.

Ujenzi ulianza mwezi Mei  mwaka 2022 na makabidhiano yamefanyika tarehe 16.09.2022. Usiri kwa wagonjwa upo kwa kutumia panzia zilizofungwa kwenye ukuta uliojengwa, ufuatiliaji wa karibu wa wagonjwa unapatikana kwa kutumia mfumo wa kuita muuguzi ambao  umefungwa, pia katikati ya wodi  kuna sehemu maalum ya kukaa wauguzi na kuna vitanda viwili karibu, kwa wagonjwa wanaohitaji huduma ya utegemezi wa hali ya juu. Pia kuna chumba kwa wagonjwa walio na magonjwa ya kuambukiza. Kila kitanda kuna vifaa vya upatikanaji wa Oksijeni. Dawa za kuua vijidudu hurahisisha  usafi na kusaidia kupunguza maambukizi ya magonjwa. Mwanga wa kutosha unapatikana kupitia taa za LED za smart.